Saturday, April 25, 2015





chadema mpango wa mungu leo kamanda wa anga freeman mbowe ananguruma bukoba mjini huo ni umati wa watu unazidi kuongezeka shikamoni bukoba mjini kwa kujitambua





HATUTALIPIZA KISASI
Mh. Mbowe alisema sisi hatutakuwa na muda wa kulipiza kisasi kutokana na yale waliyotufanyia ccm. Hata Nelson Mandela hakulipiza kisasi kwa makaburu baada ya wanaharakati wa Afrika kusini kuuawa, kupigwa, kufungwa magerezani na kufanyiwa ukatili wa kila aina. Tunakazi nzito ya ku-overhaul hii nchi kutokana uharibifu mkubwa uliofanywa na ccm kwa miaka mingi.
NB
Pongezi kubwa ni kwa watu wa mikoa ya kanda ya ziwa ( Mwaza, Shinyanga, Mara, simiyu na Kagera) kwa mabadiliko mazuri ya kimtazamo.
Na bado....>>>>>>
Tusikate tamaa tutashinda makamanda popote pale nchini.

Wednesday, March 25, 2015

Nyumba zilizojengwa juu ya bomba Buruguni kuvunjwa.

25th March 2015

Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete, jana alitembelea waathirika wa mafuriko Buguruni kwa Mnyamani na kuahidi kuwasaidia, huku akiagiza kuvunjwa kwa nyumba zitakazobainika kujengwa juu ya bomba hilo.
 
Kikwete alisema  tathmini ya nyumba ziliozojengwa juu ya bomba hilo itafanyika,  na wanaanchi watalipwa fidia zao.
 
Kadhalika, alisema bomba hilo lililosababisha mafuriko hayo litajengwa upya ili kuwezesha kupitisha maji mengi zaidi.
 
Kikwete pia ameagiza wilaya ya Ilala itoe msaada wa chakula kwa wakazi hao, pamoja na misaada mingine ya kibinadamu.
 
“Tatizo hili linashughulikiwa na litamalizika,” alisema na kuongeza: “Tatizo lililosababisha haya yote ni kuziba kwa bomba lililokuwa likipitisha maji ambalo limekutwa lina vyuma, vinu, mawe na mchanga, kwa hiyo maji yote yaliyotakiwa kupita yameshindwa kupita na kurudi kwenye makazi ya watu. 
 
Nyumba zote zitakazobainika kujengwa juu ya bomba itabidi zipishe, zitavunjwa na serikali itawalipa fidia, ila tunaomba mkiondoka msirudi tena.”
 
Alisema serikali itazungumza na wahandisi ili kuhakikisha bomba hilo linajengwa katika viwango ambavyo havitasababisha tatizo jingine kama hilo huku akiwatahadharisha wakazi wa eneo hilo kuepuka kuharibu miuondombinu na kusababisisha kutokea kwa matatizo mengine ama hayo.
 
“Haya yatakwisha, lakini ninawaomba msije mkafanya tena kama haya, ninaomba bomba litakalojengwa msiliharibu tena, mkasababisha kutokea matatizo mengine kama haya, na wale mtakaolipwa fidia msirudi tena hapa,” alisisitiza  Kikwete.
 
CHANZO: NIPASHE

Ofisi ya CUF Z'bar yateketea kwa moto.

Ofisi ya CUF Z'bar yateketea kwa moto.

25th March 2015
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam.
Ofisi za jengo la tawi la Chama cha Wananchi (CUF) Jimbo la Dimani, mkoa wa Mjini Magharibi, limeteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa ya vitu vilivyokuwamo humo ingawa thamani ya vitu hivyo haijajulikana.
 
Tukio hilo lilitokea mtaa wa Kisauni usiku wa kuamkia jana saa nane usiku.
 
Mashuhuda walisema watu wasiojulikana walifika na gari aina ya Pick-up na kuvunja mlango wa ofisi hizo na kulilipua jengo hilo kwa petroli.
 
“Majira ya saa nane usiku ilikuja gari na watu wawili walishuka katika gari hiyo na kuingia ndani huku wakisikika wakisema tayari tuondoke na baada ya kuondoka tu jengo hilo lililipuka,” alisema shuhuda mmoja aliyekuwapo katika eneo hilo.
 
Alisema baada ya kuona moto na moshi mkubwa ukiwa umetanda ndipo walipowapigia watu wa Zima Moto na walifika kuuzima.
 
Diwani wa wadi ya Tomondo, Hassan Hussen Yussuf, alisema hali inasikitisha katika harakati za kisiasa kuona Zanzibar inarejea katika siasa za chuki na uhasama.
 
“Matukio kama haya hutokea karibu na uchaguzi kwa kweli inasikitisha sana na kama halii itaendelea itakuwa hatari katika nchi,” alisema Yussuf.
 
Alisema katika jengo hilo kulikuwa na vifaa mbalimbali vya thamani na fedha taslimu za malipo ya uchukuaji wa fomu za wagombea walizolipia zimeteketea.
 
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema CUF kinalihusisha tukio hilo kuwa ni joto la uchaguzi na kuwashutumu waliofanya waliofanya tukio hilo kwani matukio kama hayo yamekuwa yakifanywa inapokaribia kipindi cha uchaguzi mkuu.
 
“Hujuma hizi zimepangwa na ni za makusudi kuchafua amani ya nchi,na hali kama hii hutokea zaidi karibu na uchaguzi na CUF hufanyiwa hujuma mbalimbali ikiwamo kuchomwa moto ofisi zetu,” alisema Bimani.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa Jeshi la Polisi 
 
linaendelea na uchunguzi.
 
CHANZO: NIPASHE

Referendum might be postponed - NEC

Referendum might be postponed - NEC

25th March 2015


NEC Chairman, retired Justice Damian Lubuva
The National Electoral Commission (NEC) yesterday said because of the snail paced progress of the Biometric Voters Registration (BVR) in Njombe Region, there is a great possibility that the referendum on the proposed Constitution may be postponed.
 
However, countering the statement from the nation’s capital Dodoma, Prime Minister Mizengo Pinda yesterday insisted that the referendum date remains April 30 as scheduled.
 
Contradicting NEC’s admission that the ongoing registration in Njombe Region is just too slow, the PM said ‘based on positive results in the updating of the voters’ registry in Njombe Region, the government believes that the referendum can be held as scheduled.’
 
Nonetheless, the Prime Minister admitted that the National Electoral Commission (NEC) will be the one to advise the government the best way forward and it is also NEC that may propose a new date based on their assessment for the exercise.
 
Speaking to reporters yesterday on the ground in Njombe Region, NEC Chairman retired Justice Damian Lubuva, said there is ‘great possibility of postponing the referendum date so as to allow voters’ registration to be completed.’
 
Lubuva said the voters’ registry is one of the major steps that are crucial in the holding of the referendum of the proposed constitution.
 
“These things go in a logical order, if A is not completed B cannot be done. We cannot hold the referendum if the updating of the voters registry is incomplete,” Justice Lubuva said. But he was hastened to add: “The date for referendum remains intact – April 30, 2015 - until we announce another date.”
 
The Chairman said based on the pace of the exercise in Njombe Region, registration is expected to come to completion on April 15, this year.
Once registration is completed in Njombe Region, he said, the regions to follow will be announced.
 
According to the NEC boss, there are more BVR equipment that are coming and if added to the current 250 units, they will reach 8,000 in total.
 
However, he did not mention the date or month when the machines will arrive in the country or clarify whether the snail’s pace of the exercise in Njombe – formerly in Iringa Region - was due to the small number of equipment available.
 
Justice Lubuva’s assertions contradicted what President Jakaya Kikwete said on March 2, this year that he was impressed by the ongoing Biometric Voter Registry (BVR) in Makambako, Njombe Region.
 
During his traditional end of the month speech for February this year, President Kikwete said from February 23 to 25, this year, the National Electoral Committee (NEC) was expected to register at least 9,541 voters but it instead registered a total of 13,042 voters.
 
The President was speaking out on the matter that has in recent months raised political temperatures in the country with members of opposition parties, with general fears that NEC might even suspend the registration exercise.
 
On February 25, this year, opposition parties forming the Coalition of People’s Constitution (Ukawa) appealed to the National Electoral Committee (NEC) to halt the ongoing registration of voters using BVR because of reported irregularities in Njombe Region.
 
Ukawa Chairman Prof Ibrahim Lipumba told journalists in Dar es Salaam then that the ongoing exercise in Njombe Region had shown errors including the possibility of one person to register in different voting stations.
“On behalf of Ukawa, I would like to call on NEC to suspend the exercise for improvement. Failure to do so may invite a political crisis,” Lipumba said.
 
But in a nutshell, the President trashed all such claims and supported the exercise during his end of the month speech.
 
President Kikwete said there were all reasons to applaud NEC for the efforts that give hope to the whole process.
 
“This clears the fears by some people that the exercise could not be successful. What we want from the commission is to see the exercise proceeding and comes to completion as expected,” the President said.
The President said as per his promise, he will make sure he does everything to help NEC to have the financial support to ensure that the exercise meets the expected target.
 
He added that he had already reminded the treasury on the importance of NEC in accomplishing the exercise as planned and that they should give it priority in the budget so as to make it a successfully exercise.
 
He called upon the political parties, religious and all non-governmental institutions to collaborate with the government and NEC in reminding and motivating the entire citizenry to register.
SOURCE: THE GUARDIAN

Thursday, March 12, 2015

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe

Chadema yambwaga Zitto mahakamani

SAFARI ya mapambano kati ya Zitto Kabwe-Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Chama chake cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imefika ukiongoni baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kutupilia mbali kesi yake namba 1 ya mwaka 2014, ya kuzuia asijadiliwe. Wanaandika Deusdedit Kahangwa na Sarafina Lidwino(endelea).
Uamuzi huo wa mahakama, unamweka Zitto njia panda ndani ya Chadema kutokana na Katiba yao kuzuia wanachama wake kuchukua hatua aliyopitia  badala ya kutumia ngazi za chama; Sasa chama kiko huru kuchukua uamuzi wowote dhidhi yake kuanzia leo.
Kanuni za kusimamia shughuli, mwenendo na maadili ya wabunge wa Chadema (2006), kifungu cha 8.0 (a) (x); zinasomeka ifuatavyo; “Chadema itashughulikia matatizo ya viongozi na wanachama kwa kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa katiba ya chama, wala hata siku moja haitashughulikia mambo kama hayo mahakamani. Mwanachama atakayeshindwa kufuata taratibu na ngazi za chama hatavumiliwa na atafukuzwa uanachama”.
Katika hukumu yake leo asubuhi, Jaji Richard Mziray amekubaliana na hoja za Chadema zilizowasilishwa na mawakili wake, wakiomba kesi hiyo ifutwe kwa madai inakiuka katiba ya chama.
Kwa mujibu wa wakili wa Chadema, Peter Kibatala, katika hukumu yake Jaji Mziray amekubaliana na hoja hizo mbili na kumtaka Zitto kukilipa chama chake gharama zote za kuendesha kesi hiyo.
“Kadiri madai haya mawili yanavyohusika, Jaji Mziray amekubaliana na mawakili wa Chadema kuhusu madai kwamba kesi iliyofunguliwa na Zitto Kabwe ilikuwa imefunguliwa kinyume cha utaratibu wa kisheria,” amesema Kibatala.
Wakili Kibatala hakusema lolote kuhusu msimamo wa Jaji Mziray dhidi ya hoja nyingine tatu walizowasilisha Mahakama Kuu. Nakala ya hukumu ya leo haikuweza kupatikana mara moja ili kutoa picha kamili ya maamuzi husika.
Katika kesi hiyo, Zitto kupitia kwa mwanasheria wake, Arbert Msendo alifungua malalamiko dhidi ya Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa pamoja na Bodi ya Wadhamini.
Mapema mwaka jana, Zitto Kabwe aliitwa na Kamati Kuuya Chadema akitakiwa kujibu tuhuma za usaliti dhidi ya chama lakini hakuitikia wito huo.
Badala yake, alifungua kesi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, akiiomba itoe amri ya kuzuia vikao vya Kamati Kuu ya Chadema kutojadili uanachama wake mpaka hapo kikao cha Baraza Kuu la Chadema kuitishwa, kupokea na kujadili na kuamua rufaa yake.
Katika rufaa yake, Zitto alikuwa anapinga uamuzi wa Chadema kumvua cheo chake cha Unaibu Katibu Mkuu.
Mnamo 21 Februari 2014, Mahakama Kuu kupitia hukumu ya Jaji John Utamwa, ilitoa zuio kwa Kamati Kuu ya Chadema kujadili na kuamua suala lolote linalomhusu Zitto.
Katika hukumu yake, Jaji Utamwa alidai kwamba, “itakuwa ni haramu kumtia hatiani mlalamikaji kwanza na kisha kumsikiliza baadaye.
Baada ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mawakili wa Chadema waliomba mapitio ya hukumu na leo maombi yao yamezaa matunda.
Awali, Wakili wa Zitto, alijibu kupinga uhalali wa maombi haya. Na baadaye, mawakili wa Chadema, Tundu Lissu na Peter Kibatala, waliwasilisha majibu yao.
Katika majibu yao ya 08 Agosti 2014 na 09 Oktoba 2014, mawakili Lissu na Kibatala, waliibua hoja tano kupinga mashitaka yaliyofunguliwa na Zitto dhidi ya uongozi wa Chadema.
Katika hoja ya kwanza, Lissu na Kibatala walidai kwamba, mashitaka ya Zitto dhidi ya uongozi wa Chadema yalikuwa ni batili kisheria kwa kuwa, yamekiuka kifungu cha 13 cha Sheria ya Kanuni ya Mwenendo wa Kesi za Madai, Sura ya 33, kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.
Kwa maoni yao, Zitto alipaswa kusajili kesi yake katika Mahakama ya Wilaya na sio Mahakama Kuu, kama alivyofanya.  
Na katika hoja ya pili, walidai kwamba, mashitaka ya Zitto dhidi ya uongozi wa Chadema yalikuwa ni batili kisheria kwa kuwa, yamekiuka kifungu cha 7(1) cha Kanuni za Masjala ya Mahakama Kuu za mwaka 2009.
Kwa maoni yao, Zitto alipaswa kusajili kesi yake katika Masjala ya Mahakama ya Wilaya na sio Masjala ya Mahakama Kuu, kama alivyofanya.
Kwa mujibu wa Kibatala, katika hukumu iliyotolewa leo na Mahakama Kuu, Jaji Mziray amekubaliana na hoja hizo mbili.
Uanachama wake
Katika mkutano wake na waandishi, Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu, amesema kwa sasa Chadema haina mahusiano yoyote ya kisiasa na Zitto.
“Kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Chadema zilizopo sasa hivi, mwanachama anayewashitaki viongozi wa chama mahakamani badala ya kufuata ngazi za kimadaraka ndani ya chama anakuwa amefanya usaliti na hivyo kupoteza sifa ya kuendelea kuwa mwanachama. Kwa hiyo, Chadema ilishamwondolea udhamini Zitto,”amesema Lissu.
Hata hivyo, mwanasheria wa Zitto, ameandika kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram kuwa taarifa kuhusu maamuzi ya Mahakama Kuu leo wamezipata kupitia mitandao ya kijamii.
“Taarifa kuhusu maamuzi ya Mahakama Kuu leo tumezipata kupitia mitandao ya kijamii kwa sababu kesi awali ilikuwa imepangwa tarehe 12.03.2015 lakini inaonekana kwenye rekodi imerudishwa nyuma na maamuzi hayo kusomwa leo bila sisi kuwa na taarifa.
“Tunafanya utaratibu tupate nakala ya maamuzi hayo ili kujua nini cha kufanya. Hatuna taarifa rasmi ya kufukuzwa Mh. Zitto Kabwe uanachama. Taratibu zote zitafuatwa pindi tukipokea taarifa rasmi kutoka mahakamani na kwenye chama. Ni matumaini yetu jambo hili halitaendeleza chuki zisizokuwa na sababu au kujenga kati ya wahusika,” amesema Msando.
Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbroad Slaa
Katibu Mkuu wa Chadema, Wilbroad Slaa

Dk. Slaa afichua mauaji dhidi yake; awataka TISS, Kikwete waachie ngazi

KIONGOZI mkuu wa upinzani nchini, Dk. Willibroad Slaa, amekoleza moto kuhusu madai ya kutokomeza maisha yake. Wanaandika Sarafina Lidwino na Deusdedit Kahangwa … (endelea).
Dk. Slaa amelieleza jeshi la polisi jijini Dar es Salaam leo (Alhamisi) kuwapo mpango wa kumuua uliokuwa unasukwa na baadhi ya viongozi wakuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na maofisa wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS).
Katibu mkuu huyo wa Chadema, ameiambia MwanaHALISI Online, muda mfupi baada ya kusajili maelezo yake kituo cha Polisi cha Kati, “Mungu bado ananipenda na anakipenda Chadema.”
Alisema, “Tumepata ushahidi usio na shaka kuhusu mpango wa kutaka kuniua. Kumekuwa na mawasiliano mazito sana kati ya maafisa usalama, viongozi wakuu wa CCM na mlinzi wangu. Mawasiliano haya yalilenga kudhuru maisha yangu.”
Amesema, “Tumebaini kwamba Idara ya Usalama wa Taifa walikuwa wanafanya ujasusi dhidi ya Chadema. Walikuwa wanatoa fedha kwa mlinzi wangu binafsi ili kumshawishi kuvujisha siri za chama. Jambo hili ni kinyume cha sheria ya kuanzishwa idara ya usalama wa taifa.
Amesema, kutaka kufanya au kutishia kuua, ni kosa la jinai, hivyo analitaka jeshi la polisi kuhakikisha mhalifu huyo, anakamatwa na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
Taarifa zinasema, aliyekuwa anashirikiana na TISS na viongozi wa CCM kutokomeza maisha ya Dk. Slaa, ametajwa kuwa ni Khalid Kagenzi.
Kwa mujibu wa mawasiliano katika simu ya Kagenzi, aliyekiri kushiriki njama za kumuua Dk. Slaa, waliokuwa wanawasiliana na Kagenzi, ni pamoja na Philiph Mangula, makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara; Gwamaka Mwang’onda na wengine kadhaa, ambao watachapishwa katika mtandao huu katika toleo lake la Jumamosi.
Akizungumza kwa uchungu na mwandishi wa gazeti hili, Dk. Slaa amesema, “Idara ya usalama wa taifa imepoteza heshima katika jamii na kuwataka viongozi wake wajiuzulu.”
Ametoa mfano wa nchini Marekani, kwamba “…ilipothibitika Rais Nixon na chama chake cha Republican walikuwa wamefanya ujasusi dhidi ya chama cha democrats, Rais Nixon alilazimika kujiuzulu. Hata CCM na idara yao ya usalama wa taifa wanafanya kosa kama hilo.”
Mwenyekiti wa CCM na ambaye ni Rais wa Jamhuri, ni Jakaya Kikwete.
Dk. Slaa amesema yeye alifika polisi kama mlalamikaji. Alitoa maelezo yake ili kuwawezesha kufanya kazi yao ya uchunguzi.
Amesema, “Sikuhojiwa kama baadhi ya watu wanavyofikiri. Mimi sio mtuhumiwa. Mimi ni mlalamikaji.”
Amesema haki zake zote zimezingatiwa alipokuwa polisi. Aliongozana na wanasheria watatu wa Chadema, Prof. Abdallah Safari, Nyaronyo Kicheere na John Mallya.
Prof. Safari, pia ni makamu mwenyekiti wa chama hicho, Tanzania Bara.
Zoezi la kuandika maelezo yake, lilitanguliwa na majadiliano kati yake na polisi ili kujenga picha ya pamoja kuhusu jambo litakalo andikwa.
Anasema, polisi waliuliza kama nataka waandike maelezo yangu wao au nataka kuyaandika mwenyewe. Nilichagua kuyaandika mwenyewe. Sheria inaruhusu hili pia.
Malalamiko yake yana kurasa tisa.
Akizungumzia wanachama watatu wa Chadema wanaoshikiliwa na polisi, Ahmed Sabula, Benson Mramba na Jacob Boniface (Diwani wa Ubungo), Dk. Slaa amesema, “Ni jambo la kusikitisha, muuaji yuko nje na waliozuia mauaji ndiyo wanaoshikiliwa.”
Habari ambazo zimepatikana baadaye zinasema, jeshi la polisi limeahidi kuwapa dhamana “makachero” hao wa Chadema kesho.

Zitto: Mimi bado mbunge.

12th March 2015
Chapa
Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe.
Siku moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kumvua uanachama Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, Zitto amesema hajapewa taarifa rasmi, hivyo ataendelea kuwa mbunge.
 
Pamoja na kauli hiyo ya Zitto, viongozi wa Chadema wamesema hawatahangaika kumwandikia barua kumjulisha hatua zilizochukuliwa na chama hicho dhidi yake.
 
Zitto akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam, alisema ataendelea na kazi yake ya ubunge kwasababu hajapewa taarifa rasmi na Chadema kuhusu uamuzi uliochukuliwa wa kumvua uanachama.
 
“Sina taarifa rasmi kilichotokea na kama mnavyoona naendelea na vikao vya kamati kama kawaida na leo (jana) nitakuwa na watu wa Benki Kuu (BoT), TRA (Mamlaka ya Mapato Tanzania) na AG  (Mwanasheria Mkuu wa Serikali), Ijumaa nitakwenda Kigoma jimboni kwangu kwa ajili ya kazi zangu, niliwahidi wananchi wangu nitakwenda kabla ya kwenda bungeni, kimsingi mimi bado ni mbunge,” alisema.
 
Licha ya Chadema kutangaza kumvua uanachama, Zitto jana aliendesha vikao vya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) kama kawaida.
 
Zitto alisema hawezi kujibishana na chama chake kwani hajalelewa katika maadili kama hayo na kwamba kitu muhimu kwake ni kazi ya kuwatumikia Watanzania.
 
“Mimi huwezi ukanilinganisha na mbunge yeyote katika kazi ambazo nimekuwa nikizifanya, siasa kwangu ni ‘issues’ tofauti na watu wengine ambao siasa zao ni kugombana na watu, kwangu hizi ni changamoto, nakomazwa,” alisema.
 
Alisema ifahamike kuwa maamuzi yoyote lazima yafanywe kwa kikao na hayawezi yakaamuliwa na mtu mmoja.
 
“Maamuzi yoyote yanayotolewa ni ‘process’ (mchakato) kwa sababu hata kwa maamuzi ya chama kuna suala la kumwandikia barua Spika wa Bunge naye ajiridhishe, kwa hiyo mimi bado ni mbunge ambaye nilichaguliwa kuanzia mwaka 2005 hadi sasa na nitaendelea kuwatumikia Watanzania,” alisema. 
 
LISSU; HATUTAMWANDIKIA BARUA ZITTO 
Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu, alisema chama hicho hakitahangaika kumwandikia barua Zitto kumjulisha uamuzi wake kwa kuwa anajua alishakiuka Katiba ya chama kwa kushtaki hivyo uanachama wake unakoma mara moja.
 
Lissu alisema jana kuwa: “Sisi hatuhitaji kumfahamisha kwa sababu anajua adhabu ya kukiuka Katiba, tutaandika barua kwenye mamlaka husika siyo kwake.”
 
Alisema Chadema kitamwandikia barua Katibu wa Bunge na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), kuwafahamisha uamuzi huo.
Hata hivyo, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah, alipoulizwa na NIPASHE jana alisema, hadi jana jioni alikuwa hajapokea barua ya Chadema juu ya kumtimua uanachama Zitto.
 
 WABUNGE WAMLILIA
Baadhi ya wabunge wamezungumzia kuvuliwa uanachama kwa Zitto, wengine wakimshauri kuwa kama hajaridhika anaweza kukata rufaa zaidi mahakamani.
 
Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila, alisema hawezi kuingilia uhuru wa Mahakama kwa kuwa ndiyo mhimili wa kutoa haki.
 
Hata hivyo, alisema Zitto ana nafasi ya kukata rufaa ngazi ya juu ya Mahakama kama hajaridhika na uamuzi huo. 
 
LUGOLA: CHADEMA WAMEKOSEA  
Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola, alisema amepokea kwa mshtuko taarifa za Mahakama kutupa shauri la Zitto, akieleza kuwa Chadema nayo haijatumia busara kumfukuza. 
 
“Nimeshtushwa na kusikitishwa zaidi kwa kitendo cha Chadema kumvua uanachama kwa sababu mahali ambapo sisi CCM tumefika tulikuwa tunahitaji upinzani imara ambao unatunyima usingizi ili  tuisimamie vyema serikali, katika mazingira ambayo tunahitaji upinzani imara kama Chedema sidhani kama wamechukua uamuzi wa busara,” alisema. 
 
Lugola alisema uimara wa Chadema hautapatikana kwa kumfukuza Zitto, bali kwa kuvumiliana na kutafuta muafaka ndani ya chama hicho pale zinapotokea. 
 
Alisema CCM inahitaji Chadema imara ili iwe makini katika kuwatumikia wananchi na kwamba kwa kumfukuza Zitto, Chadema na CCM vitadhohofika kwa kuwa vitakosa mtu makini wa kuikosoa.
 
“Mchango wake ulikuwa ni mkubwa na wangeweza kuiga CCM ambayo ina watu ambao walianza kampeni za urais mapema, lakini hatujawafukuza, tumewaonya. Chadema isiangalie mabaya ya CCM iyachukue mazuri tuliyonayo,” alisema. 
 
SERUKAMBA: INADIDIMIZA DEMOKRASIA 
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Peter Serukamba, alisema uamuzi wa Chadema unadhohofisha demokrasia nchini.  
 
Alisema Katiba ya nchi ilipaswa kuyatazama ili kukomesha udikteta wa demokrasia nchini, akisema kwa Zitto ni miongoni mwa wabunge wenye ushawishi mkubwa, hivyo Chadema walipaswa kutomtimua. 
 
MWIGULU: NIMESIKITISHWA
 Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, alisema amesikitishwa na taarifa za kuenguliwa uanachama Zitto ndani ya chama alichoanzia siasa, alichokitumikia kwa jasho na mali, alichowekeza muda na akili yake kwa zaidi ya miaka 19.
 
Mwingulu ambaye aliandika taarifa hiyo katika mtandao wake wa Facebook, alisema Zitto amekuwa chachu ya mabadiliko kwa vitendo kwa Taifa.
 
“Uwezo wa kisiasa wa Zitto adhabu yake siyo kumfukuza, demokrasia ni lazima itumike, nakusihi kijana mwenzangu, mwanasiasa mwenzangu na mchumi mwenzangu kuwa, Taifa linakuhitaji sana wakati huu tunapopambana na ufanyaji kazi kwa mazoea na kuleta mabadiliko kwa vitendo, usikate tamaa Watanzania watakuhesabia mema kwa yote unayoyafanya kwa ajili ya Taifa letu,” alisema Nchemba ambaye pia ni Mbunge wa Iramba Magharibi.
 
MZIRAY: CHADEMA WAMEFANYA MAAMUZI YA JAZBA
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Peter Kuga Mziray, alisema Chadema imefanya maamuzi ya kumvua uanachama Zitto kwa jazba kwa sababu hali hiyo haiwezi kusaidia kuviimarisha vyama vya upinzani kupambana na chama tawala.
 
“Inaonekana kumekuwa na jazba na kutafutana katika maamuzi haya, siasa za kuviziana na kukomoana siyo nzuri, Zitto amefanya kazi nzuri sana ndani ya Chadema kulikuwa na sababu gani kufanya maamuzi haraka ya kumvua uanachama,” alisema
Mziray  pia ni Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha APPT Maendeleo.
 
 ADC : CHADEMA WANGEMSAMEHE ZITTO
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance For Change (ADC), Doyo Hassan Doo, alisema uamuzi uliochukuliwa na Chadema ni wa haraka kwani wangeweza kulitazama suala hilo kibinadamu na kumsamehe.
 
“Hatukatai  Chadema wamefuata katiba yao kumfukuza Zitto, lakini si vibaya kama wangemsamehe, sisi hatuungi mkono hii tabia mbaya iliyoanza kujengwa na baadhi ya vyama vya siasa kufukuzana fukuzana,” alisema.
 
ACT: TUNAMKARIBISHA ZITTO 
Katibu Mkuu wa Chama cha  Alliance for Change and Transparency (ACT- Tanzania), Samson Mwigamba, alimshauri Zitto asikate rufaa kwa kuwa atapoteza muda, badala yake achukue uamuzi wa kujiunga na ACT.
 
 “Tunatambua mchango wa Zitto katika Taifa hili, siasa zake ni tofauti na siasa za watu wengine, ni za kistaarabu, uzalendo na anapenda maelewano na watu wote, hivi sasa kila chama kitapenda kumkimbilia ila atambue kwamba ACT pekee ndiyo chama kinachoweza kumfanya atimize ndoto zake za kisiasa,” alisema Mwigamba.
 
Juzi Lissu, alitangaza Zitto kuvuliwa uanachama kwa madai ya kukiuka katiba ya chama kifungu cha 8(a) (x) ambacho kinaeleza kuwa, mwanachama yeyote akifungua kesi mahakamani dhidi ya chama akishindwa katika kesi hiyo anakuwa amejifukuzisha uanachama.
 
CHANZO: NIPASHE

PAC yaagiza CAG uchunguzi wa milioni 699/- za Tanesco.

12th March 2015
Chapa
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe.
Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imemwagiza Mdhibti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi kubaini zilikopotelea Sh. milioni 699 zilizotolewa na Wizara ya Fedha kwenda Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ambazo hazijulikani ziliko sasa.
 
Aidha, PAC imeagiza Tanesco kuwasilisha katika ofisi ya Bunge mikataba yote ya kampuni zinazozalisha umeme nchini ambazo zimeingia nayo mikataba ili kupitiwa upya na kuwa kumbukumbu kwa Bunge.
 
Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe, alitoa maelekezo hayo jana katika kikao baina ya kamati hiyo na menejimenti ya Tanesco na kusema kumekuwa na mvutano kuhusu Sh. milioni 699 zilizotolewa na Hazina kwenda Tanesco.
 
Zitto alisema inawezekana fedha hizo zimetolewa kwa Tanesco, lakini zimetumika vibaya au Hazina wamezitoa kwa mtu tofauti, hali ambayo imekuwa ikileta mkanganyiko ambao unahitaji kufanyiwa uchunguzi.
 
Kaimu Afisa Mkuu wa Fedha Tanesco, Anetha Chegula, alisema fedha hizo zinadaiwa kutolewa na Hazina tangu mwaka 2012 kwenda Tanesco kwa ajili ya kusaidia miradi ya umeme, lakini hazijafika katika shirika hilo licha ya Hazina kuonyesha kuwa zilishatolewa.
 
Chengula alisema wamekuwa wakiitaka Hazina kuonyesha vielelezo vinavyoonyesha kuwa fedha hizo zimepelekwa Tanesco, lakini hadi mwaka jana Hazina haikufanya hivyo huku Tanesco ikifanya uchunguzi katika akaunti zake bila kuziona fedha hizo.
 
Akizungumzia mikataba ya makampuni ya Agrecco, Symbion, Songas na IPTL , alisema ipelekwe haraka ofisi za Katibu wa Bunge ili iwe kumbukumbu kwa Bunge.
 
Wabunge walisema tozo ya uendeshaji wa mitambo (capacity charge) iangaliwe upya kwa sababu inaingiza gharama kubwa kwa Tanesco, hivyo kushindwa kufikia malengo ya kujiendesha badala yake kuendelea kutegemea serikali kulisaidia.
 
Mbunge wa Nkasi, Ally Kessy, alisema ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini ni kwa Tanesco kuchukua hatua ya kuinunua mitambo ya umeme inayomilikiwa na kampuni zinazozalisha umeme na kuiuzia Tanesco kwa bei ya juu.
 
Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Felchesmi Mramba (pichani), alisema Songas inalipwa Sh. bilioni 8.562 za tozo ya uendeshaji, IPTL Sh. bilioni 4.302 na Aggrecco Sh. bilioni 1.600 kwa mwezi. Mramba alisema Aggreco imekuwa ikiiuzia Tanesco umeme kwa Dola za Marekani senti 40 na IPTL senti 23 huku Tanesco ikiuza umeme huo kwa senti Dola za Marekani 26.
 
CHANZO: NIPASHE

Vilio, vilio, vilio.

12th March 2015
Basi la abiria la Majinje Express lenye namba za usajili T438 CDE likiwa limegongana na lori la mizigo lililokuwa limebeba kontena ambalo liliangukia basi hilo na kuua watu 42, eneo la Changarawe, barabara kuu ya Iringa Mbeya jana. Picha: George Tarimo
Vilio na simanzi jana vilitawala kwenye mji wa Mafinga, wilaya ya Mufindi, mkoani Iringa, kufuatia watu 42 kufariki dunia na wengine 23 kujeruhiwa, baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupata ajali.
 
Ajali hiyo ilitokana na basi hilo la kampuni ya Majinje Express lenye namba za usajili T.438 CDE kugongana uso kwa uso na lori la mizigo ‘semitrela’ namba T698 APJ na kisha kontena lililokuwa kwenye lori hilo kulifunika basi lilokuwa na abiria.
 
Miongoni mwa waliofariki ni pamoja na dereva wa basi hilo, huku dereva wa lori akielezwa kuwa mahututi katika Hospitali ya Wilaya ya Mafinga.
 
Waliofariki wametajwa kuwa ni Ester Emmanuel, Lusekelo Enock, Jeremia Watson, Digna Solomon, Frank Chiwango, Luten Sanga, Teresia Kamiyage na Dotto Katuga.
 
Wengine ni Esta Fide, Pauline Justine, Mbamba Ipyana, Catherine Mwajengo, Zera Kasambala, Rebeka Kasambala Mr. Musa, Shadrack Msigwa, Mathias Justine, Mr. Elias na Juliana Bukuku.
 
Wamo pia Christina Lyimo, Martin Haulo, Dominick Mashauri, Esta Willy, Lucy Mtega, Erick Shitind, Edwaga Kamiyage, Frank Mbale, Mustafa Ramadhani, Kelvin Odubi, Mr. Osward, Omega Mwakasege, Upendo William, Iman Mchange, Charles Lesenga, Mr. Neto Sanga, Pili Vincent, Mr. Hamad, Ed Erick, Daud so Stones na Jacob Doketa.
 
Lori hilo linalomilikiwa na kampuni ya Cipex, lilikuwa kiliendeshwa na Baracka Gabriel, kutoka Iringa kwenda Mbeya.
 
Ajali ilitokea majira ya 3:30 asubuhi, eneo la Changarawe katika barabara kuu ya Iringa-Mbeya.
 
Basi hilo lilikuwa likitokea mkoani Mbeya kwenda jijini Dar es Salaam na lori hilo lilikuwa likitokea Dar es Salaam kwenda nchi jirani ya Zambia.
 
Habari kutoka eneo hilo zinaeleza kuwa ajali hiyo imechangiwa kwa kiasi kikubwa na ubovu wa barabara na mwendo kasi wa basi hilo.
 
Kwa mujibu wa habari hizo, eneo ambako ajali hiyo imetokea kuna shimo kubwa.
 
Habari hizo zinaeleza kuwa, dereva wa lori alifanikiwa kulikwepa shimo hilo, lakini dereva wa basi alipojaribu, alishindwa kulimudu basi hilo na hivyo kutumbukia. 
 
Baada ya kutumbukia kwenye shimo hilo, magari hayo yalijaribu kupishana na wakati yakipishana, kontena lililokuwa kwenye lori hilo lililiangukia basi na kusababisha vifo hivyo.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, alithibitisha kutokea ajali hiyo mbaya.
 
Alisema ajali hiyo kama zilivyo nyingine, zimechangiwa na uchakavu wa miundombinu ya barabara.
 
“Ndugu zangu wanahabari, hii ni ajali kama ilivyo ajali nyingine. Kwa sababu, imetokea sehemu mbaya. Na pia uchakavu wa barabara unachangia na siyo ajali ya kujitakia,” alisema Kamanda Mungi.
 
Baadhi ya majeruhi wa ajali hiyo, waliliambia NIPASHE kwamba, awali basi hilo lilikuwa katika mwendo kasi.
 
Kutokana na hali hiyo, walimuita kondakta wa basi hilo na kumtaka amwambie dereva apunguze mwendo, lakini hakufanya hivyo.
 
Kevin Hamfrey, ambaye alikuwa akitokea Mbeya kwenda jijini Dar es Saalam aliitaka serikali kuangalia upya suala la miundombinu kwani imekuwa chakavu na ndiyo iliyochangia ajali hiyo.
 
Musa Mwasega alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi, ambao ulisababisha dereva kushindwa kulimudu gari na hivyo kusababisha kugongana uso kwa uso na lori hilo.
 
“Kiukweli ajali hii ni mbaya sana. Na sisi wenyewe baada ya kuona dereva anajaribu kulimudu, tulijua lazima kuna kitu kitatokea kwa sababu awali mwendo kasi ulikuwa siyo wa kawaida,” alisema Mwasega.
 
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mufindi, Boaz Peter, alithibitisha kupokea miili ya watu 42 na majeruhi 23.
 
Alisema hadi sasa wanafanya jitihada ili ndugu watambue miili ya marehemu na kwenda kuichukua.
 
Peter alisema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Mufindi, wakati majeruhi wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mufindi.
 
Alisema kati ya miili 42,  32 ilipelekwa Hospitali Kuu ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kwa ajili ya kuhifadhiwa kutokana na chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Mufindi kuwa finyu.
 
Kutokana na hali ya majeruhi wengine kuwa mbaya, wawili walichukuliwa na gari la wagonjwa ya wilaya hiyo na kuhamishiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.
 
 Kati ya waliofariki dunia, wanaume ni 37, wakati wanawake ni watano.
 
Baadhi ya wananchi wa mji mdogo wa Mafinga, ambao hawakupenda majina yao kuandikwa gazetini, walisema mara kwa mara wamekuwa wakitoa kilio chao kwa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) na baadhi ya viongozi wa ujenzi wa barabara wilaya ya Mufindi, lakini kimekuwa hakisikilizwi.
 
Badala yake, wamekuwa wakijibiwa kuwa suala hilo litapelekwa kwa viongozi husika.
 
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza, aliiagiza Tanroads kuanza kushughulikia uchakavu wa barabara hiyo mara moja.
 
“Msiba huu ni wa watu wote, siyo wa mtu mmoja, nimesikitika sana kusikia kuwa asubuhi kuna ajali ilitokea  eneo la Changarawe nje kidogo ya mji wa Mafinga na nilivyosikia nimekuja mara moja kuangalia ni jinsi gani tutafanya ili kuwasaidia ndugu hawa, ”alisema Masenza.
 
Rais Jakaya Kikwete amemtuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Masenza, na kuwahakikishia wafiwa wote kuwa yuko pamoja nao na kuwaombea majeruhi wote wapone haraka ili waendelee katika shughuli zao za ujenzi wa taifa. 
CHANZO: NIPASHE

Mbio za uchaguzi mkuu wagombea watizamwe hivi!


Watu wakilinda masanduku ya kura,
Wakati Uchaguzi mkuu unakaribia, porojo zilizozagaa mitaani na taarifa za vyombo vya mawasiliano na mitandaoni ni majina ya  wagombea wakijadiliwa na kusifiwa kuwa wana kila sifa ya kuongoza taifa na jimbo hivyo ndiyo wanaohitajika kuipokea kura ya ndiyo.
 
Si mbaya kuwafahamu watakaowaongoza lakini ni vyema kujua zaidi uwezo wa marais, madiwani  na wabunge wajao, je historia zao zinasemaje, wana haiba gani (personality/ character) pia  uadilifu wao ukoje?
 
Katika kuwachunguza viongozi watarajiwa kuna baadhi ya vidokezo vinavyowazungumzia viongozi na sifa zao kama vinavyonukuliwa kutoka kwenye machapisho na mihadhara ya Mhubiri wa Kimataifa hayati Dk. Myles Munroe, wa Huduma ya Bahamas Faith Ministry, ambavyo kiongozi kwa mtizamo wake anahisi analazimika kuwa navyo.
 
Akizungumza katika moja ya mihadhara wakati wa uhai wake  (alifariki mwishoni mwa mwaka jana  katika ajali ya ndege) aliainisha kuwa kiongozi haimaaniisha kuwa mtu aliyefanya mambo makubwa ya kutisha tena mwenye mafanikio makubwa, kwa mfano pengine tajiri wa kwanza duniani Bill Gates wa Marekani ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Computer ya Microsoft.
 
Japo ni bilionea na mashuhuri lakini si kwamba unapozungumzia viongozi wote si lazima wawe na sifa za utajiri, umaarufu au kuwa wakipekee duniani sivyo anasema la muhimu ili uwe kiongozi ni lazima uwe na maono, muadilifu mwenye haiba pamoja na karsima au karama.
 
Akianza na maono anazungumzia suala la kuwa na maono na malengo yanayotekelezeka tena uwezo wa akili za kuyaweka mambo yaende sawa na kuwahamasisha wale anaowaongoza kuleta mafanikio na kutekeleza malengo wanayojiwekea.
 
 Kiongozi awe wa kitaifa, mbunge, diwani, mkuu wa mkoa, wilaya  au mkurugenzi wa shirika la umma ama la binafsi ni lazima aweze kufanikisha malengo na maono aliyoyaweka yawe ya kampuni, kiwanda ama serikali au jimbo ni sharti awe na uwezo wa kuyatimiza kwa ushindi unaoonekana.
 
Unaposema huduma za afya kwa kila Mtanzania, kama ndilo lengo basi watu waone miundombinu, wataalamu, vifaa , dawa na kuhakikisha kuwa wananchi wanapona na kampeni zimefanikiwa kutokomeza maradhi. 
 
Mhubiri huyu wa kimataifa anasema kabla hujajiingiza kwenye kutangaza nia ya kuwa kiongozi chunguza uadilifu wako. 
 
Uadilifu ni ile hali ya ukweli (faithfulness and diligence) kwa nafsi zao, Mungu wao na wale wanaotarajia kuwaongoza. Kadhalika ni kwa kiasi gani wana kasrima.
 
Haya ni mahojiano yako na Mungu wako.Anataka kiongozi ajiulize yukoje kiuaminifu? “Jipime katika maeneo haya- hofu ya Mungu, kutumia na kulinda mali zako na za umma, fedha unazokabidhiwa, utendaji kazi, uhusiano na wenzako, familia yako na ujue kama ni mwaminifu ama vipi. 
 
Huu mtihani wa uadilifu (diligence) baina yako  na Mungu maana unayeyajua majibu ni wewe binafsi.”
 
Haitoshi watu kusema mgombea huyu amefanya mambo makubwa , ana uwezo huu ama ule. Sifa za wapambe hazijengi wala hazikupi uadilifu huo ni uchunguzi  wako binafsi na Mungu unayemwamini. 
 
UONGOZI NI NINI
Dk Myles Munroe anajibu kuwa unajumuisha mambo mengi lakini , ni muhimu katika kuendeleza shughuli na michakato duniani lakini pia  unahitajika ili kuwafunza na kuwaandaa wengine watakaoongoza sekta na mapambano ya kuleta mabadiliko na hali bora za maisha ya watu na kuufanya ulimwengu kuwa mahala pazuri pa kuishi.
 
Anakumbusha kuwa hakuna neno moja linaloweza kutumiwa kumzungumzia anayetakiwa kuwa rais, mbunge, diwani au kiongozi  maana mambo ni mengi na hakuna sifa pekee ya kumweleza kiongozi. 
 
Hata hivyo Munroe anaona kuwa kiongozi ni huyo  ambaye anateuliwa ama kuchaguliwa kuliongoza kundi timu, shirika na taifa.
Anaelezwa kuwa kiongozi anatakiwa kuwa na karisma au  mwenye uwezo wa kufanya maamuzi muhimu, mwenye mvuto na haiba anayeweza kuwashawishi wengine.
 
Kwa kifupi uongozi ni ‘charism’ au karama ambayo inahusisha haiba kubwa na ni kipaji kutoka kwa Mungu.Kadhalika ni uwezo wa kimamlaka unaoweza kuwasiliana na wengine kikamilifu kuhamasisha wengine kufanya yale yaliyokusudiwa na kuona kuwa yanaleta manufaa.Si kuibuka na kueleza kauli mbiu za kufurahisha lakini zisizotekelezeka. Kwa ujumla kiongozi awe na uwezo wa kushawishi wengine na kuwabadilisha kwa namna bora .
 
VIGEZO VYA KIONGOZI
Ili uwe kiongozi ni lazima uwe na kundi unaloshirikiana nalo linalofuata maelekezo au nyayo zako na lenye imani na maono, malengo na maongozi yako.Kama kiongozi una jukumu kwa watu wako wawe wapiga kura, wafanyakazi wataasisi la kuwaongoza kwa weledi na haki, uhuru na kwa maadili na uadilifu pia na kuonyesha karama yako.
 
Vyeo vya kimamlaka vinavyohusisha kutukuzwa kama “mheshimiwa, bosi, chifu,mkurugenzi, baba, mtukufu” hakika havikufanyiwa kuwa kiongozi bora wakati mwingine vyaweza kuwa kejeli.
 
YAKUFANYA
Kuwa kiongozi bora unahitajika kujiweka sawa na viwango vya juu na vya wakati wa sasa vya marais au viongozi wengine wakuu duniani na kikanda, hivyo fuatilia nyendo za viongozi wenzako duniani wanavyopambana na kuondoa matatizo mbalimbali. 
 
Kwa mfano utasikia Baba Mtakatifu Papa Francis anatembelea makundi ya watu maskini, anazungumza na kujichanganya nao mitaani.
 
Anafahamu nini anachotakiwa kufanya kuwagusa wote anaowaongoza na ikibidi kuwafikia kwa kuwa kuongoza ni ‘karama’ kipaji alichopewa na Mungu analazimika kwenda kwa watu duni pengine  wasiofikiwa wala kukumbukwa na viongozi!
 
Kama ni rais angalia jinsi wale wa kalba yako (marais wenzako) wanavyofanya, mikakati na mipango ya maendeleo ya kuyawezesha mataifa yao kung’ara kwenye ramani ya dunia.
 
KUSOMA
Rais, mbunge ama mkurugenzi unalazimika kusoma machapisho ya aina mbalimbali kuanzia ripoti za kimataifa, za kiuchumi za Afrika, Umoja wa Mataifa, habari za mbadiliko ya tabia nchi. Kadhalika jifunze kuwa mkweli siyo kuongea mambo ya kudandia bila kuwa na vyanzo vya uhakika.
 
Soma magazeti ya kimataifa na ya kitaifa, tizama habari na matukio mbalimbali duniani kwenye televisheni, soma machapisho ya mitandao mbalimbali na unapozungumza kuwa na mamlaka yaani uwe unaelewa mambo. Kuwa mtu wa kutumia watalaamu na kufanya tafiti uwe gwiji la uelewa.
 
Lazima ufahamu habari za kibiashara na uchumi duniani kupitia machapisho mbalimbali, angalia viongozi , watizame wenzako katika mashirika mbalimbali duniani na katika tasinia za kimataifa na kikanda ujue wanafanyaje? Jipime wewe uko wapi katika ngazi za viongozi kitaifa na kimataifa? Waheshimiwa fanyeni tafiti  si kukurupuka na kusema chama chetu kitashinda kwa wimbi la tsunami ama wakati wa kukiondoa chama tawala ni huu, umetafiti? Umezungumza na wananchi?
 
Kutafiti, kujisomea na kufahamu mambo mengi kutakupa mwelekeo na jinsi ya kuwa kiongozi bora na mweledi huku ukijijengea uzoefu wa kipekee kukabiliana na changamoto unazozifanyia kazi.
 
Kwa hiyo mnapoelekea kwenye uchaguzi mkuu jaribuni kujichunguza  na kujiweka kwenye viwango na mjiulize ninastahili?  Na nyie wapambe na mashabiki angalie tunayemtaka anatufaa? Ana vigezo? Au mkishahongwa mmeridhika. Mnawajibu wa kumtafakari kwa viwango hivyo.
 
 
CHANZO: NIPASHE

Wanawake wataishi kwa hofu vijijini hadi lini


ChapaDunia inapoadhimisha Siku ya Wanawake duniani mamia ya wanawake vijijini wanaishi kwa hofu kwani ni walengwa wakuu wa kila sababu ya mauaji. Wanasingiziwa kuwa wachawi, wanadaiwa wasababisha mikosi, maadui wa mvua lakini pia wanageuzwa viambato vya kutengeneza dawa kwani miili yao inachanganywa mambo mengine kuleta utajiri na mafanikio.  

Mauji ya wanawake yamekithiri maeneo ya Ukanda wa Ziwa mikoa ya Mwanza, Geita, Shinyanga, Kagera na Simiyu na kila mara imeshuhudiwa wazee, mabinti na hata walemavu wakiuawa kwa visingizio mbalimbali vinavyohusisha uchawi.

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (HLRC) cha jijini Dar es Salaam, kinasema wanawake zaidi ya 1,000 wameuawa mwaka jana na kwamba kuanzia mwaka 2010 hadi sasa zaidi ya wanawake 3,000 wanaotuhumiwa kuwa ni wachawi wamepoteza maisha wakiwa na umri kati ya miaka 50 hadi 80.

Wauaji huwashambulia kwa mapanga, visu, kuwachoma moto wakiwa hai mabaki ya miili yao huteketezwa pia wala asitokee mtu wa kuwatetea.

Taarifa zinaeleza kuwa mauji hutokea usiku wa manane, milango huvunjwa kwa mawe makubwa ama wauaji huvizia na kuingia vyumbani wanapolala wanawake, ambao bila msaada wanakatwa kwa mapanga, visu, kuchomwa moto na nyumba zao kupigwa kiberiti.

Wanadaiwa ni wauaji wa watoto  Mikoa ya Kanda ya Ziwa ni kitisho mwanamke anaweza kunyanyaswa akatumiwa radi au mvua ikanyesha juu ya paa lake, akang’olewa mazao shambani, mifugo yake ikauliwa na pia anaweza kuchomwa ndani ya nyumba pamoja na wajukuu zake nyakati za usiku.

Yote hufanyika kwa wasio na hatia kwa vile hakuna ukweli kuwa ni wachawi. Mwalimu Mbuke Mayala wa mkoani Tabora, anasema katika mahojiano ya simu kuwa mauji haya yanachochewa na serikali kushindwa kudhibiti wauaji na kukomesha matendo hayo maovu kwa vile haitafuti kiini cha watu kuendelea kuamini uchawi na kuwa watumwa wa imani za kishirikina.

“Muda wote imeendelea kuwatumia polisi, mahakama na sheria lakini bila kukomesha tabia zilizo ndani ya mioyo ya watu kuendekeza uchawi na kuamini kulogwa kwa muda mrefu.”

Mwalimu Mbuke mkazi wa kijiji cha Witangh’olo mkoani Tabora, anaeleza zaidi kuwa ushirikina umejikita zaidi kwenye ukanda huu ambao wengi hawana elimu , wanaamini imani za kimila na matambiko ya kijadi na pia hakuna huduma za afya zinazoweza kutumiwa kupunguza vifo na kukabiliana na maradhi kama Virusi Vya Ukimwi (VVU), vifo vya watoto na wazazi wao, malaria na pia magonjwa yanayoweza kuepukwa.

Anasema waganga ndiyo wanaotegemewa lakini hawafahamu chanzo wala hawana tiba za magonjwa ambayo kama kungekuwa na huduma za afya wananchi wangehudumiwa na kupona.

Mbuke anasema elimu duni inasababisha jamii kuamini mambo kama kuzaa watoto mapacha ni mkosi, mtoto anayezaliwa akitanguliza makalio analeta balaa na wanalazimika kufanyiwa matambiko.

Kadhalika watu wanaendeleza mila za kurithi wajane , kuwatakasa na kuoa wanawake kwa imani mbalimbali wengine wakiamini wana mikono ya pesa au wanazaa watoto wa kiume.

Ushirikina wa kuua albino umewaumiza zaidi wanawake na watoto wadogo. Hivi karibuni Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, ilitoa taarifa ya kuionya Tanzania kuhusu mauaji ya albino na kulaani kitendo cha kuwateka na kuwaua watoto albino.

 Kamishna wa Haki za Binadamu wa UN Zeid Ra’ad Al Hussein, katika taarifa hiyo alisema mauaji yataongezeka kwa vile kinakaribia kipindi cha uchaguzi Oktoba mwakani. Idadi ya wanawake albino waliouliwa ni wengi ikilinganishwa na wanaume.

Hawa huuliwa kwa vile hawawezi kujitetea na hawana nguvu. Lakini pia ni ukweli kuwa wanaonewa na jamii muda wote.

Kwa mujibu wa Chama cha Albino Tanzania kwa kipindi cha miaka 15 iliyopita zaidi ya albino 75 wameuliwa licha ya kwamba hazikutolewa takwimu kijinsia lakini idadi kubwa ni wanawake na wanaweza kufikia karibu 40.Hawa wanaozungumziwa ni wale ambao taarifa zao zinafahamika.

Wapo waliochinjwa kwa siri na haikujulikana hadi leo hatima yao.
Lakini cha kushangaza zaidi waliotiwa hatiani ni wafungwa 10 pekee kati yao wapo waliohukumiwa kifungo cha maisha na wenye adhabu ya kunyongwa hadi kufa.

Ili kutokomeza mauaji ya albino, kuua wanawake na kuendeleza imani za kishirikina serikali inawajibika kutoa elimu shuleni na ile ya kuhamasisha jamii kuachana na ushirikina.

Kadhalika kujenga miundo mbinu na kutoa huduma za afya na kushirikiana na wadau wengine kutokomeza mauaji ya Watanzania wasio na hatia kwa kisingizio chochote.

Mauaji ya wanawake na wazee huambatana na watu wanaowalisha watuhumiwa dawa za kubaini ‘wachawi’ waganga wanadai ukitumia dawa hizo lazima utaonyesha dalili zinazohusiana na matendo hayo.

Kupitia elimu serikali na wadau wakomeshe tabia za baadhi ya watu wanaozurura mitaani kujidai wanaumbua wachawi. Pia sheria ziwepo na mienendo hiyo idhibitiwe ili kuwanusuru wanawake wengi wanaouliwa bila hatia.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

Mtei na ndoto za Chadema kushika dola 2015

11th March 2015
Chapa
Edwin Mtei.
“Nimeandaa dume la ng’ombe, Oktoba 31, mwaka huu. Ukija hapa siku hiyo nakukaribisha katika sherehe kubwa nitakayoiandaa…nitachinja dume na kuwaaga viongozi wa Chadema watakaokuwa wamechaguliwa kushika dola kusherehekea ushindi.”
 
Hiyo ni kauli ya matumaini. Ni kauli inayotoka mdomoni mwa Muasisi na Mwenyekiti mstaafu wa Chadema, Edwin Mtei, akielezea jinsi anavyoona na matarajio yake kwa Uchaguzi Mkuu ujao.
 
“Nakukaribisha siku hiyo na huu ndio mwaliko wako, uje kusherehekea ushindi wa Chadema hapa nyumbani, kabla ya viongozi hao kwenda kuapishwa Dodoma.”
 
Alikuwa akizungumza na mwandishi wa makala hii nyumbani kwake eneo la Shangarai, wilayani Tengeru, Mkoa wa Arusha.
 
Kauli ya Mzee Mtei imekuja siku chache baada ya Katibu wa Chadema, Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa, mwishoni mwa mwezi ulipita kuwa chama hicho kimeandaa mikakati ya kutwaa dola Oktoba, mwaka huu.
 
Golugwa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Arusha, anasema hawataki tu kuwa na chama maarufu ila kuchukua dola, tena sio miaka mingi ijayo ila Oktoba mwaka huu.
 
Akiweka msisitizo, Mtei anasema uchaguzi mkuu ujao ndio utadhihirisha matakwa ya demokrasia.
 
Anasema Chadema itachagua mgombea makini mwenye maadili na sifa ya kuongoza nchi. Mtu mwenye upeo na mawazo ya maendeleo kwa wananchi na taifa.
 
Ukawa
 
Akizungumzia kuhusu Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), anasema mgombea wa Chadema atashindanishwa na wagombea wengine kutoka umoja huo kwa mujibu wa makubaliano yao ya kusimamisha mgombea mmoja.
 
“Mimi ninaamini katika demokrasia ya ushindani, ndiyo demokrasia yenyewe kwamba kila chama kichague mgombea mmoja na kumshindanisha ili kumpata mgombea bora atakayekubalika,” anasema.
 
Hata hivyo,  anasema, “hatutakubali kuangusha wengine ili kumpata mmoja, lakini tukimpata mmoja huyo aliyeachwa tutamweleza aendelee kubaki kwenye chama.”
 
Anasema anaamini katika siasa au demokrasia za ushindani na kama kuna chama hakina mwelekeo huo basi kinaweza kufa.
 
Kuhusu uchaguzi mkuu, anasema, “Tunatarajia utakuwa uchaguzi huru, kila lazima ashiriki na kikubwa zaidi kupiga kura ili kuhakikisha kwamba wanatumia uhuru wao,” anasema.
 
Akitahadharisha kuhusu uvunjifu wa demokrasia katika uchaguzi, haraka haraka anakionya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuacha kutumia pesa za walipakodi ambazo baadhi ya wagombea wao waliziiba zamani.
 
Anasema kwa muda mrefu chama hicho kimekuwa kikivuruga chaguzi mbalimbali na kuzifanya kuwa sio huru na wakati mwingine kimekuwa kikitumia mbinu za kupeleka mafisadi na watu walioiba fedha za walipa kodi kuhakikisha wagombea wa CCM wanapita.
 
“Wasitumie pesa zetu ambazo walituibia zamani na wengine ambao wamezificha nje ya nchi kuhonga watu wetu ili wasishiriki,” anasema na kucheka kidogo, na kuongeza, “hata zile fedha za IPTL ni zetu.”
 
Anasema kuna baadhi ya watu walisema wasusie uchaguzi mkuu, lakini anaona lazima washiriki na kutekeleza demokrasia yao.
 
Anasema anayo matumaini makubwa ya Chadema kuungwa mkono na watu wengi na hiyo inatokana na jinsi walivyokihamasisha na kukiuza chama hicho kwa wananchi na sasa kinakubalika.
 
“Kutokana na mwamko wa chama chetu na jinsi tulivyowahamasisha wananchi; na CCM inavyotumia nguvu kubwa kupambana na Chadema, ikiwa ni pamoja na nguvu ya ufisadi kuhonga wanachama ili kuleta mgongano ndani ya chama, nadhani wananchi kwa kuelewa hilo wanaweza kutuunga mkono katika harakati zetu za kutwaa dola Oktoba  2015,” anasema.
 
Anasema nafasi zote za wagombea katika uchaguzi mkuu kuanzia udiwani, ubunge na urais, wataungwa mkono na wananchi na kushinda na ishara hii inatokana na matokeo mazuri ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji ulifanyika Desemba 14, mwaka jana.
 
Mathalan, anasema, “katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa, tumeonyesha kuwa sisi ndio chama kinachokubalika na sasa tutaendelea katika ngazi kata, majimbo na taifa.”
 
Anasema mikakati mingi ya kukinadi chama ndiyo ilisaidia kukifikisha hapa kilipo hali ambayo inawafanya waendelee kusomba watu wote kuanzia ngazi ya mashina, kitongoji, kijiji, mtaa, kata, tarafa, jimbo hadi taifa, na hii ndiyo kielelezo cha ushindi.
 
Changamoto BVR
 
Anaangalia changamoto katika mfumo wa kielektroniki wa kuandikisha wapiga kura (BVR) kama teknolojia ambayo haiwezi kuepukika katika nyakati hizi za maendeleo ya kisayansi na kiteknolojia.
 
Hata hivyo, anasema matatizo yanayotokana na mfumo huo ni kwa sababu ya uwezo mgogo wa serikali na nchi.
 
Anasema serikali haikuweza kuandaa wataalam wenye uwezo wa kuzifanyia matengenezo mashine hizo au namna ya kuziendesha.
 
“Ni lazima na mwelekeo ulivyo, sasa ni lazima tutumie vifaa hivyo, kama shida itakuwa muda hautoshi, wanaweza kuongeza muda hadi Julai au Agosti, ili kuwapa watu wengi nafasi ya kujiandikisha na hivyo kupiga kura.
 
CCM imeshindwa?
 
Kuhusu CCM, Mzee Mtei hamung’unyi maneno, anasema moja kwa moja kwamba chama hicho kikongwe kimeshindwa na kupoteza mvuto kwa Watanzania. Kwa kifupi anasema hakikubaliki isipokuwa kwa wale wachache wenye maslahi nacho.
 
Anataja kwa mfano, Watanzania wanakufa kwa njaa kuanzia Ukerewe, mkoani Mwanza hadi Rombo, mkoani Kilimanjaro.
 
Anasema wakati wananchi wanakufa njaa, yapo mashamba mengi na makubwa yameshindwa kulima, huku fedha nyingi ambazo zinatolewa na washirika wa maendeleo haziwafikii wahusika.
 
Migogoro ndani ya chama
 
Anasema inapotokea inakiimarisha chama, na inatakiwa kutatuliwa kwa misingi ya kidemokrasia.
 
“Unajua kila mwanasiasa lazima awe ambitious, atake ukubwa kuliko pale alipo; na hii ni demokrasia, lazima kuwa na ushindani,” anasema.
 
Pamoja na siasa, Mzee Mtei anajishughulisha na kilimo cha mahindi, kahawa na ufugaji wa nguruwe na ng’ombe wa maziwa.
 
Anasema kwa mfano, mwaka huu amavuna tani 1, O30 za mahindi katika shamba lake la hekari 95.
 
Anasema ameuza mahindi hayo na kutenga magunia machache kwa ajili ya chakula chake kwa mwaka mzima, magunia 40 kwa ajili ya chakula cha nguruwe wake 37 yakiwemo madume mawili.
 
CHANZO: NIPASHE

Wednesday, March 4, 2015

Mkurugenzi wa TGNP, Lilian Liundi
Mkurugenzi wa TGNP, Lilian Liundi

Wanawake wataka mafanikio zaidi

WAKATI Tanzania ikiungana na mataifa mengine duniani kusherehekea Siku ya Wanawake, Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), umeainisha changamoto kadhaa zinazowakabiri wananwake nchini. Anaandika Sarafina Lidwino... (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika maadhimisho ya miaka 20 ya azimio la Ulingo wa Beijing, Mkurugenzi wa TGNP, Lilian Liundi amesema, siku hii hukutanisha wanaharakati wote wanaotetea haki za wanawake ili kujadili mafanikio na changamoto na jinsi ya kukabiliana nazo.
Liundi amesema, pamoja na mafanikio waliyoyapata hususani katika nyanja za kisiasa ya kuongezeka kwa viongozi wanawake, lakini bado kuna mapungufu katika uwezeshaji katika uongozi wao.
Amesema, mbali na kuongezeka kwa shule, bado hazikidhi mahitaji, majengo yapo lakini waalimu ni wachache na wengi hawana ujuzi, mabweni hakuna, umbali mrefu unaosababisha wasichana kupata mimba.   
Kwa mujibu wa Liundi, Serikali imejitahidi kujenga vituo vya afya, lakini changamoto iliyopo ni wahudumu hakuna wala dawa. Hivyo waathirika wakubwa ni wanawake, haswa wakati wa kujifungua, hukosa huduma na kupoteza maisha.
Lihundi amesema, mzigo wa majukumu unamwelemea sana mwanamke, hivyo kukosa muda wa kushiriki katika shughuri za kimaendeleo na uchumi.
Ameongeza kuwa bado kuna maendeleo ya vitu wakati wananchi walio wengi wanazidi kuathirika na mfumo uliopo wa kiuchimi; mabenki yapo lakini hakuna anayepata mkopo, soko limekuwa holela, vitu visivyokuwa na viwango vimejaa sokono, wakati bidhaa zetu zinakosa soko.
“Sekta zisizo rasmi, ambapo wanawake wengi ndio wapo huko haijaweza kumkomboa mwanamke na kumtoa katika duru ya umaskini. Ajira bado ni tatizo kubwa kwa wanawake Tanzania,” amesema Liundi.