Wednesday, March 25, 2015

Nyumba zilizojengwa juu ya bomba Buruguni kuvunjwa.

25th March 2015

Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete, jana alitembelea waathirika wa mafuriko Buguruni kwa Mnyamani na kuahidi kuwasaidia, huku akiagiza kuvunjwa kwa nyumba zitakazobainika kujengwa juu ya bomba hilo.
 
Kikwete alisema  tathmini ya nyumba ziliozojengwa juu ya bomba hilo itafanyika,  na wanaanchi watalipwa fidia zao.
 
Kadhalika, alisema bomba hilo lililosababisha mafuriko hayo litajengwa upya ili kuwezesha kupitisha maji mengi zaidi.
 
Kikwete pia ameagiza wilaya ya Ilala itoe msaada wa chakula kwa wakazi hao, pamoja na misaada mingine ya kibinadamu.
 
“Tatizo hili linashughulikiwa na litamalizika,” alisema na kuongeza: “Tatizo lililosababisha haya yote ni kuziba kwa bomba lililokuwa likipitisha maji ambalo limekutwa lina vyuma, vinu, mawe na mchanga, kwa hiyo maji yote yaliyotakiwa kupita yameshindwa kupita na kurudi kwenye makazi ya watu. 
 
Nyumba zote zitakazobainika kujengwa juu ya bomba itabidi zipishe, zitavunjwa na serikali itawalipa fidia, ila tunaomba mkiondoka msirudi tena.”
 
Alisema serikali itazungumza na wahandisi ili kuhakikisha bomba hilo linajengwa katika viwango ambavyo havitasababisha tatizo jingine kama hilo huku akiwatahadharisha wakazi wa eneo hilo kuepuka kuharibu miuondombinu na kusababisisha kutokea kwa matatizo mengine ama hayo.
 
“Haya yatakwisha, lakini ninawaomba msije mkafanya tena kama haya, ninaomba bomba litakalojengwa msiliharibu tena, mkasababisha kutokea matatizo mengine kama haya, na wale mtakaolipwa fidia msirudi tena hapa,” alisisitiza  Kikwete.
 
CHANZO: NIPASHE

Ofisi ya CUF Z'bar yateketea kwa moto.

Ofisi ya CUF Z'bar yateketea kwa moto.

25th March 2015
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam.
Ofisi za jengo la tawi la Chama cha Wananchi (CUF) Jimbo la Dimani, mkoa wa Mjini Magharibi, limeteketea kwa moto na kusababisha hasara kubwa ya vitu vilivyokuwamo humo ingawa thamani ya vitu hivyo haijajulikana.
 
Tukio hilo lilitokea mtaa wa Kisauni usiku wa kuamkia jana saa nane usiku.
 
Mashuhuda walisema watu wasiojulikana walifika na gari aina ya Pick-up na kuvunja mlango wa ofisi hizo na kulilipua jengo hilo kwa petroli.
 
“Majira ya saa nane usiku ilikuja gari na watu wawili walishuka katika gari hiyo na kuingia ndani huku wakisikika wakisema tayari tuondoke na baada ya kuondoka tu jengo hilo lililipuka,” alisema shuhuda mmoja aliyekuwapo katika eneo hilo.
 
Alisema baada ya kuona moto na moshi mkubwa ukiwa umetanda ndipo walipowapigia watu wa Zima Moto na walifika kuuzima.
 
Diwani wa wadi ya Tomondo, Hassan Hussen Yussuf, alisema hali inasikitisha katika harakati za kisiasa kuona Zanzibar inarejea katika siasa za chuki na uhasama.
 
“Matukio kama haya hutokea karibu na uchaguzi kwa kweli inasikitisha sana na kama halii itaendelea itakuwa hatari katika nchi,” alisema Yussuf.
 
Alisema katika jengo hilo kulikuwa na vifaa mbalimbali vya thamani na fedha taslimu za malipo ya uchukuaji wa fomu za wagombea walizolipia zimeteketea.
 
Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Mawasiliano ya Umma wa CUF, Salum Bimani, alisema CUF kinalihusisha tukio hilo kuwa ni joto la uchaguzi na kuwashutumu waliofanya waliofanya tukio hilo kwani matukio kama hayo yamekuwa yakifanywa inapokaribia kipindi cha uchaguzi mkuu.
 
“Hujuma hizi zimepangwa na ni za makusudi kuchafua amani ya nchi,na hali kama hii hutokea zaidi karibu na uchaguzi na CUF hufanyiwa hujuma mbalimbali ikiwamo kuchomwa moto ofisi zetu,” alisema Bimani.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mjini Magharibi, Mkadam Khamis Mkadam, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa Jeshi la Polisi 
 
linaendelea na uchunguzi.
 
CHANZO: NIPASHE

Referendum might be postponed - NEC

Referendum might be postponed - NEC

25th March 2015


NEC Chairman, retired Justice Damian Lubuva
The National Electoral Commission (NEC) yesterday said because of the snail paced progress of the Biometric Voters Registration (BVR) in Njombe Region, there is a great possibility that the referendum on the proposed Constitution may be postponed.
 
However, countering the statement from the nation’s capital Dodoma, Prime Minister Mizengo Pinda yesterday insisted that the referendum date remains April 30 as scheduled.
 
Contradicting NEC’s admission that the ongoing registration in Njombe Region is just too slow, the PM said ‘based on positive results in the updating of the voters’ registry in Njombe Region, the government believes that the referendum can be held as scheduled.’
 
Nonetheless, the Prime Minister admitted that the National Electoral Commission (NEC) will be the one to advise the government the best way forward and it is also NEC that may propose a new date based on their assessment for the exercise.
 
Speaking to reporters yesterday on the ground in Njombe Region, NEC Chairman retired Justice Damian Lubuva, said there is ‘great possibility of postponing the referendum date so as to allow voters’ registration to be completed.’
 
Lubuva said the voters’ registry is one of the major steps that are crucial in the holding of the referendum of the proposed constitution.
 
“These things go in a logical order, if A is not completed B cannot be done. We cannot hold the referendum if the updating of the voters registry is incomplete,” Justice Lubuva said. But he was hastened to add: “The date for referendum remains intact – April 30, 2015 - until we announce another date.”
 
The Chairman said based on the pace of the exercise in Njombe Region, registration is expected to come to completion on April 15, this year.
Once registration is completed in Njombe Region, he said, the regions to follow will be announced.
 
According to the NEC boss, there are more BVR equipment that are coming and if added to the current 250 units, they will reach 8,000 in total.
 
However, he did not mention the date or month when the machines will arrive in the country or clarify whether the snail’s pace of the exercise in Njombe – formerly in Iringa Region - was due to the small number of equipment available.
 
Justice Lubuva’s assertions contradicted what President Jakaya Kikwete said on March 2, this year that he was impressed by the ongoing Biometric Voter Registry (BVR) in Makambako, Njombe Region.
 
During his traditional end of the month speech for February this year, President Kikwete said from February 23 to 25, this year, the National Electoral Committee (NEC) was expected to register at least 9,541 voters but it instead registered a total of 13,042 voters.
 
The President was speaking out on the matter that has in recent months raised political temperatures in the country with members of opposition parties, with general fears that NEC might even suspend the registration exercise.
 
On February 25, this year, opposition parties forming the Coalition of People’s Constitution (Ukawa) appealed to the National Electoral Committee (NEC) to halt the ongoing registration of voters using BVR because of reported irregularities in Njombe Region.
 
Ukawa Chairman Prof Ibrahim Lipumba told journalists in Dar es Salaam then that the ongoing exercise in Njombe Region had shown errors including the possibility of one person to register in different voting stations.
“On behalf of Ukawa, I would like to call on NEC to suspend the exercise for improvement. Failure to do so may invite a political crisis,” Lipumba said.
 
But in a nutshell, the President trashed all such claims and supported the exercise during his end of the month speech.
 
President Kikwete said there were all reasons to applaud NEC for the efforts that give hope to the whole process.
 
“This clears the fears by some people that the exercise could not be successful. What we want from the commission is to see the exercise proceeding and comes to completion as expected,” the President said.
The President said as per his promise, he will make sure he does everything to help NEC to have the financial support to ensure that the exercise meets the expected target.
 
He added that he had already reminded the treasury on the importance of NEC in accomplishing the exercise as planned and that they should give it priority in the budget so as to make it a successfully exercise.
 
He called upon the political parties, religious and all non-governmental institutions to collaborate with the government and NEC in reminding and motivating the entire citizenry to register.
SOURCE: THE GUARDIAN