Thursday, February 5, 2015

Ewura yazidi kushusha bei ya mafuta

Ewura yazidi kushusha bei ya mafuta

4th February 2015

























Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), imetangaza kushusha bei za mafuta ya taa, petroli, dizeli nchi nzima kuanzia leo.
 
Aidha, kushuka kwa bei hizo kutapelekea kushuka kwa gharama za umeme na wapo kwenye mchakato wa uratibu kati ya Ewura na Wizara ya Nishati na Madini, ili kuangalia  gharama za uzalishaji na namna ya kupunguza bei ya umeme.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Felix Ngamlagosi, alisema mabadiliko hayo yametokana na kushuka kwa bei ya mafuta katika soko la dunia.
 
Alisema bei ya mafuta masafi katika soko la dunia kwa petroli, dizeli na mafuta ya taa zimepungua kwa asilimia 35 hadi 40, kuanzia Julai na Desemba, mwaka jana.
 
Alisema mafuta hayo yameshuka kwa takribani dola 440 kwa tani kwa mafuta petroli, dizeli imeshuka kwa dola 304 kwa tani na mafuta ya taa kwa dola 324 kwa tani.
 
Akizungumzia kushuka kwa bei hizo katika soko la ndani, alisema petroli imeshuka kwa Sh. 187 kwa lita sawa wakati dizeli imeshuka kwa Sh. 139 kwa lita na mafuta ya taa yameshuka kwa Sh.177.
 
“Mabadiliko haya ya bei yametokana na kushuka kwa bei za mafuta katika soko la dunia na kupungua kwa gharama za uagizaji mafuta, bei za mafuta katika soko la ndani zingepungua zaidi,” alisema na kuongeza kuwa 
 
“Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta kwenye mabango yanayoonekana bayana na yakionyesha bei ya mafuta punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika na ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika.”
 
Alisema bei za petroli kwa Dar es Salaam imeshuka kutoka Sh. 1,955 hadi 1,768,  dizeli Sh. 1,846 hadi 1,708 na mafuta ya Sh. 1,833  hadi 1657.
Arusha petroli imeshuka hadi 1,852, dizeli Sh. 1,791 na mafuta ya taa Sh. 1,741.
 
Dodoma bei ya petroli sasa itakuwa Sh. 1,827, dizeli Sh. 1,766 na mafuta ya taa Sh. 1,715

BVR yaibua hofu bungeni

BVR yaibua hofu bungeni

5th February 2015


























Bunge limeonyesha kutoridhishwa na hatua ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), kuamua kuendesha zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapigakura kwa kutumia mfumo mpya wa kielektroniki (BVR), bila  kuwashirikisha wadau wakuu, hali ambayo imeelezwa kuwa inaweza kusababisha machafuko katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu nchini.
 
Hatua hiyo ya Nec inadaiwa kuchukuliwa kinyume cha makubaliano yaliyofikiwa kati yake na wadau wakuu wa uchaguzi, ambao ni vyama vya siasa.
 
Kutokana na hatua hiyo ya Nec, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu, aliitisha kikao cha Kamati ya Uongozi ya Bunge jana asubuhi ili kujadili suala hilo kabla ya Bunge kuishauri serikali nini kifanyike.
 
Uamuzi huo wa Zungu ulitokana na hoja iliyotolewa na Mbunge wa Kuteuliwa (NCCR-Mageuzi), James Mbatia, bungeni jana, ambaye alitaka Bunge lisimamishe shughuli zake za jana asubuhi ili kujadili suala hilo aliloliita kuwa ni la ‘dharura.’
 
Mbatia alisema Nec juzi ilikutana na kuamua kuanza kundesha zoezi hilo katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Njombe bila wadau wakuu kushirikishwa kama walivyokubaliana kwenye meza ya mazungumzo.
 
Alisema makubaliano hayo yalifikiwa katika kikao cha wadau wakuu kilichofanyika Januari 8, mwaka huu, kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) chini ya Mwenyekiti wake, John Cheyo, ambacho Nec walialikwa.
 
Mbatia alisema katika kikao hicho, Nec iliwahakikishia kuwa zoezi hilo lina changamoto kubwa na kwamba, lingeanza upya Januari 15, mwaka huu.
 
Alisema zoezi hilo lilianza mwanzoni mwa Juni, mwaka jana, lakini halikufanikiwa, pia likafanyika tena mwishoni mwa mwezi huo, katika maeneo ya mkoa wa Rukwa, vilevile likafeli. Alisema wakakubaliana kuwa Nec na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (Zec) wakutane na kujadili kwa pamoja kisha wawaelimishe wadau namna zoezi hilo litakavyofanyika kwa kutumia BVR ili wakubaliane kama lina maslani kwa taifa au la.
 
Mbatia alisema walifikia makubaliano hayo kwa kuwa iwapo jambo hilo halitaendeshwa vizuri nchi inaweza kuingia kwenye machafuko.
Hata hivyo, alisema juzi Nec ilikutana na kuanza kufanya utaratibu wa kuendesha zoezi hilo katika mikoa hiyo bila wadau wakuu kushirikishwa kama walivyokubaliana kwenye meza ya mazungumzo.
 
Alisema katika kikao hicho, walikubaliana kuwa zoezi hilo lihakikishe linafanyika kwa uadilifu, uaminifu na kwa pande zote kushirikishwa.
Mbatia alisema wadau waliokutana katika kikao hicho, wanatoka vyama vyote vya siasa, kikiwamo Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambacho kiliwakilishwa na Makamu wake Tanzania Bara, Philip Mangula.
 
Alivitaja vyama vingine vilivyoshiriki kikao hicho cha wadau kuwa ni pamoja na Chadema, iliyowakiloshwa na Katibu Mkuu wake, Dk. Willibrod Slaa, CUF (Prof. Ibrahim Lipumba), NCCR-Mageuzi (James Mbatia), TLP (katibu mkuu wake) na vyama vingine visivyokuwa na uwakilishi bungeni.
 
Alisema jambo hilo lina maslahi mapana kwa umma na kwamba, katika kikao hicho, Nec ilieleza mambo mengi sana.
 
"Tukawashauri kwa nia njema kwamba, ni bora tukae, tuzibe ufa kabla ya kujenga ukuta tuaminiane," alisema Mbatia.
 
Alisema pia waliisisitiza kuwa Nec ulazima wa kulifanya jambo hilo ili kuhakikisha kwenye uchaguzi mkuu malalamiko yanapungua na kuhakikisha yaliyotokea katika uchaguzi mkuu wa Kenya, Ghana, Msumbiji na Malawi yasitokee nchini.
 
Kutokana na hali hiyo, alisema kwa mujibu wa kanuni ya 47, Bunge linapaswa kutekeleza matakwa ya ibara ya 63 (2) ya katiba ya nchi inayotambua kazi ya Bunge kuwa ndiyo chombo kikuu cha kuisimamia na kuishauri serikali ili zoezi hilo lifanyike kwa uadilifu na kwa ufanisi mkubwa kuepuka mtatizo yaliyotokea katika nchi hizo yasitokee hapa nchini.
 
"Na hakuna jambo jema kama kuaminiana katika jambo lenye maslahi kwa taifa," alisema Mbatia.
 
Akijibu hoja hiyo, Zungu alisema anakubaliana kwamba, jambo hilo ni la muhimu, kukaa pamoja na Bunge kuwa ni chombo cha kuishauri serikali.
Hivyo, akaiagiza serikali kuanzia wakati huo kukaa pamoja na Mbatia wakalijadili kwenye Kamati ya Bunge ya Uongozi.
 
Hata hivyo, Kamati ya Uongozi, imelipeleka suala hilo kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala ili likafanyiwe kazi.
Katika kikao hicho, serikali imesisitiza kuwa imeshatoa fedha za kutosha kwa ajili ya BVR.

Tanzania haitaandika Katiba Mpya

Kaimu Mwenyekiti wa JUkwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Hebron Mwakagenda
Kaimu Mwenyekiti wa JUkwaa la Katiba Tanzania (JUKATA), Hebron Mwakagenda

Tanzania haitaandika Katiba Mpya

KATIBA Mpya inayotokana na maoni ya wananchi, tayari imeshindikana. Bunge Maalum la Katiba, limeshindwa kufanya kazi iliyotumwa. Limeishia mivutano, malumbano, kejeli, vijembe, matusi, ubaguzi na mipasho.
Yote hayo yamebarikiwa na aliyekuwa mwenyekiti wa Bunge Maalum, Samwel Sitta.
Hebron Mwakagenda, makamu mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) amesema, Sitta amewanyima wananchi fursa muhimu ya kujiandikia katiba yao.
“Kuwepo kwa wabunge na wawakilishi ndani ya Bunge Maalum, kulikinzana na dhana ya katiba kama zao la wananchi wenyewe. Wawakilishi na wabunge wamechochea sana kuvunjwa kwa dhana kuwa katiba, ni mkataba mkuu kati ya watawala na wananchi,” ameeleza Mwakagenda.
Amesema, “Bunge na Baraza la Wawakilishi ambavyo ni vyombo toto vya Katiba, havikuwa na mamlaka ya kuzaa katiba.”
Aidha, kitendo cha Muungano wa Kutetea Katiba ya Wananchi (UKAWA) na baadhi ya wajumbe kutoka kundi la 201 na kususia bunge hilo ni pigo kubwa kwa mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya nchini.
Kitendo cha kupindishwa kwa Kanuni za Bunge Maalum katika hatua ya uzinduzi; jambo ambalo limesababisha rasimu ya Katiba kuwasilishwa bungeni kabla ya Bunge kuzinduliwa, ni ishara kuwa kulikuwa na hila za serikali juu ya mchakato huu.
Ushauri wa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Muungano, Jaji Frederick Werema ukupingana na ule uliotolewa na aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Othman Masoud Othman, juu ya mamlaka ya Bunge Maalum.
Othuman alisema, Bunge Maalum halina mamlaka ya kugeuza rasimu ya katika kutoka muundo wa serikali tatu hadi mbili zinazopigiwa chapuo na CCM.
Badala ya kutafuta suluhu, maoni ya Othman yalinyamaziwa au kubezwa; hali iliyomfanya Othman kujiengua kutoka kamati ya uandishi.
Othman ni miongoni mwa wajumbe waliopiga kura ya hapana katika Katiba Inayopendekezwa.
Lakini badala ya kuheshimu haki yake ya kupiga kura kwa utashi wake, liliibuka wimbi la kidikteta la ndani ya chama tawala kumshambulia na kumdhihaki. Hatimaye Othuman alifutwa kazi.
“Badala ya Katiba Mpya kuwa chanzo cha maridhiano, muafaka na maelewano, imeishia kuwa zao la uhasama. Kwa sababu hiyo na nyingine, Katiba inayopendekezwa haiwezi kuitwa Katiba Mpya,” ameeleza Mwakagenda.
Ni vema wananchi wasome na kuelewa Katiba Inayopendekezwa na kuilinganisha na Rasimu ya Katiba ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 (2005) na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 (2010).
Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya wananchi imeshindwa kupatikana, kwa kuwa Rais Jakaya Kikwete alijiingia katika mradi huu bila maandalizi na utashi wa kisiasa.
Alijiingiza katika utafutaji wa katiba mpya kwa kusukumwa na mvumo wa wanasiasa wa upinzani, vyombo vya habari na wanaharakati wengine. Ndiyo sababu hivi sasa ameungana na chama chake kupuuza maoni ya wananchi katika kutunga katiba mpya

CHADEMA: Serikali ya JK inavunja sheria ya kura ya maoni

Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu
Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu

CHADEMA: Serikali ya JK inavunja sheria ya kura ya maoni

SERIKALI itakuwa inatenda kosa la jinai kujiingiza katika kushawishi wananchi kuiridhia katiba inayopendekezwa ambayo imepitishwa na Bunge Maalum la Katiba.
Kwa mujibu wa Sheria ya Kura ya Maoni ya mwaka 2013, kazi ya kutangaza katiba inayopendekezwa kwa nia ya kuelimisha wananchi itaratibiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi na siyo chombo kingine chochote.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu alisema kitendo chochote kitakachofanywa na Ikulu au ofisi nyingine yoyote ya serikali, kinacholenga kushawishi wananchi wairidhie katiba, ni kuvunja sheria.
Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema Ikulu itakuwa imejiingiza katika uvunjaji wa sheria za nchi kutekeleza mkakati wa kuhamasisha Watanzania kuikubali na kuipigia kura ya NDIO katiba inayopendekezwa.
“Kitendo cha serikali ya Rais Kikwete, mawaziri wake na maofisa wa serikali yake kutaka kutumia fedha za umma kufanya kampeni kwa katiba inayopendekezwa na CCM kwa Watanzania sio tu ni matumizi mabaya ya fedha za umma bali pia ni kosa la jinai kwa mujibu wa sheria za nchi hii,” alisema Lissu.
Amesema Lissu kwamba Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Salva Rweyemamu kusema, “Kila kitu kinakwenda kwa sheria, hata hizo fedha zitatolewa na serikali kama ambavyo ilitoa za kugharamia Bunge Maalum” hakutoshi kuhalalisha uvunjaji wa sheria. Kwenyewe ni kinyume cha sheria.
Amesema maadili na sheria za uchaguzi zikiwemo Sheria ya Kura ya Maoni ya 2013, Sheria ya Uchaguzi, Sura ya 343 na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya mwaka 2010 zitahusika na masuala yoyote yanayohusu matumizi ya fedha wakati wa kura ya maoni.
“Sheria zetu za uchaguzi na maadili zinakataza kitendo kinachofanywa na Ikulu. Ni kosa la jinai kwa mijibu wa Sheria ya Gharama za Uchaguzi ya 2010, sehemu ya tano ya hii sheria inazungumzia vitendo vinavyokatazwa,” alisema Lissu.
Lissu amesema sheria hiyo inataja mwenendo usiostahili kuwa ni: Wakati wa mchakato wa uchaguzi, kampeni za uchaguzi au uchaguzi, kitendo kinachokatazwa ni kile mtu ambaye kabla au kipindi cha kampeni, moja kwa moja au kwa namna nyingine yoyote kupitia kwa mtu mwingine yeyote.
Au kwa niaba yake anatoa, anakopesha au anakubali kutoa au kukopesha au anatoa, anaahidi au kumpatia au anajaribu kumpatia fedha yeyote au kitu kingine chochote chenye thamani mpiga kura.
“Au mtu yeyote kwa niaba ya mpiga kura yeyote au mtu mwingine yeyote kwa nia ya kumshawishi mpiga kura kupiga kura au kuacha kupiga kura au kumrubuni mtu yoyote kuacha kutenda kitendo hicho katika kura za maoni na uchaguzi, sheria imekataza,” amesema Lissu.
Akifafanua kuhusu kifungu cha cha 21 (1) (a) cha sheria ya gharama za uchaguzi kuwa malipo yasiyofaa: Kila mtu ambaye kwa njia ya rushwa yeye mwenyewe au kumtumia mtu mwingine yeyote kwa niaba yake ama kabla
Wakati wa uchaguzi kwa uwazi au kwa kificho anatoa au anaandaa au analipa kwa ujumla au kwa sehemu gharama ya kuandaa kinywaji au chakula au mahitaji ya mtu yeyote kwa nia ya kumshawishi mtu huyo au mtu mwingine yeyote kupiga kura sheria inakataza.“Hivyo Rais ameonesha kwa mwenendo au kwa maneno ya Salva kwamba anataka kushiriki mchakato wa kupata katiba, hivyo wanakatazwa pia na kifungu cha 25 cha sheria ya gharama za uchaguzi, hawawezi kuhalalishwa haya makosa yanatendwa na Rais hayawezi kuwa 
halali.
“Matendo ya kihunikihuni ya namna hii yatawafanya watu waingie barabarani na kuchoma moto mabunge, kama ilivyotokea Burkina Faso wiki iliyopita. Uhuniuhuni wa namna hii, dharau kwa wananchi za namna hii ndizo zinazovunja amani,” alisema Lissu.
Lissu alisema ni vizuri Tume ya Taifa ya Uchaguzi izungumze hadharani kama wanachokifanya Ikulu na chama cha CCM ni halali.
Alisema Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) unakusudia kupeleka malalamiko NEC kuhusu mpango huo wa Serikali ya Rais Kikwete kutaka kutumia fedha za umma kutekeleza mpango wa kushawishi wananchi waikubali katiba inayopendekezwa kwa kupiga kura ya NDIO.
Waziri Lazaro Nyalandu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu

GMS: Ninashangaa wanaonihujumu wanalindwa

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Awadh Ally Abdallah ameiambia MwanaHALISI Online kwamba wakati anapewa adhabu kupitia vyombo vya habari Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu ameendelea “kujizuia” isivyoeleweka kuwaondoa washindani wake kampuni ya Wengert Windrose Safaris Limited (WWS).
“Mimi ninayefanya shughuli zangu kwa shida kutokana na vikwazo nilivyowekewa na mshindani, kinyume cha sheria, ninaadhibiwa. Yule ambaye anatufanyia fujo na kuikosesha mapato serikali, ambaye ilishaelekezwa aondolewe kwa nguvu, analindwa na Waziri. Inasikitisha sana,” amesema.
Awadh amesema Waziri Nyalandu anajua vizuri mezani kwake tangu Mei mwaka jana, alishauriwa na wataalamu wa Idara ya Wanyamapori kumuondoa WWS kwa kung’ang’ania kitalu isivyo halali kisheria, lakini hajachukua hatua yoyote.
“Tulikuwa na professional hunter tuliyemwajiri maalum ili kuongoza safari ya wageni wetu kuwinda mwaka 2012. Jukumu lake ni pamoja na kusimamia uwindaji usioharibu wanyama na mazingira yao,” alisema.
Awadh alisema “wageni wetu hawakuwa peke yao. Walikuwepo maofisa wa wanyamapori ambao wamesomea kazi pamoja na walinzi pia walikuwepo. Wote hawa walikuwa wapi wakati makosa yanayodaiwa kufanywa yalipokuwa yakitendwa.
“Sisi tunasikitika kutangaziwa adhabu hewani kama vile tupo mbali na Wizara. Hatujajulishwa lolote ili nasi tutoe maelezo yetu. Hakuna mawasiliano yoyote tuliyoyapata kutoka Wizara ya Maliasili,” alisema kwa mshangao.
“Hadi sasa hatujafahamishwa rasmi hicho kinachotajwa na vyombo vya habari kuwa tumekitenda. Inakuaje mtu anapewa adhabu bila ya kujulishwa kosa lake,” anahoji.
“Baada ya kusikia tunavyotuhumiwa, niliomba maelezo ya tuhuma kwa sababu mimi sina uwezo wa kuingia bungeni na kusema pale ninapotuhumiwa. Sijajibiwa kitu hadi leo… wananichukulia hatua kali pasina kunipa nafasi ya kujitetea. Hizi sheria katili hivi zinatoka wapi jamani,” amesema.
Awadh anasema amemwandikia barua Spika wa Bunge, Anne Makinda kumuomba ufafanuzi wa tuhuma dhidi yake ambazo zilitolewa bungeni na Waziri Kivuli wa Maliasili na Utalii, Mchungaji Peter Msigwa.
Hata hivyo, Awadh anashangaa kutojibiwa lolote mpaka sasa hali inayothibitisha kuwepo mpango wa kumchafua bila ya kupewa nafasi ya kujitetea.
Julai 11, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, alitangaza kufuta leseni ya kuendesha vitalu vya uwindaji ya kampuni ya GMS kwa maelezo kuwa imevunja sheria ya uwindaji.
Siku mbili baadaye, GMS kupitia kampuni ya uwakili ya Haki Kwanza, imesema hatua hiyo ni kutekeleza matakwa ya washindani wao kampuni ya Wengert Windrose Safaris (WWS) ambayo imekuwa ikiwania kitalu kilichomilikishwa kwa GMS mwaka 2013
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva

Vitambulisho vya kupigia kura, mradi feki

MRADI wa vitambulisho vipya vya kupigia kura nchini, umeshindwa kabla ya kuanza. Vitambulisho vipya vya taifa vitaandaliwa kupitia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR).
Mfumo huu unatumika kuchukua au kupima taarifa za mtu za kibaiolojia au tabia za mwanadamu na kuzihifadhi katika kazidata (database) kwa ajili ya utambuzi.
Gharama za mradi huu unaotarajiwa kugharimu zaidi ya Sh. 293 bilioni. Umepangwa kuanza Septemba 2014.

Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu Damian Lubuva, ameeleza wahariri wa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam, mpango huo ni “sehemu ya mchakato wa kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura.”
Kushindwa kwa mradi huu, kumesababishwa na yafuatayo:
Kwanza, mfumo huu unahitaji kuwapo kwa vifaa vya kisasa – komputa, kamera, kifaa cha kuchukulia alama za vidole na mashine ya kutotoa vitambulisho (printa).
Vifaa hivi vinavyohitajika, vinatumia umeme, tena wa uhakika. Katika maeneo mengi ya nchi hayana umeme. Machache yaliyobahatika kuwa na umeme, yamekuwa yakikumbwa na mgawo wa mara kwa mara.
Mpaka sasa, serikali kupitia Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO), wameshindwa kufikisha umeme nchi mzima. Taarifa za serikali zinaonyesha, ni asilimia 30 ya watu wote ndiyo waliobahatika kupata umeme.
Nchini Bolovia, mashine hizi zilitumika katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2009. Lakini kabla ya kuziingiza katika uchaguzi, taifa hilo lilitoa mafunzo kwa maelfu ya maofisa wa usimamizi wa uchaguzi kwa miezi kadhaa.
Hata hivyo, siku ya uchaguzi ilipowadia, mitambo yao ilikwama kufanya kazi. Zilitolewa sababu mbili: Virusi kuingilia mfumo wa utendaji wa komputa na kufuta baadhi ya taarifa na kutokuwapo mtandao wa uhakika wa intaneti, hasa vijijini. Matatizo kama hayo yanaweza kutokea nchini.
Pili,tekronojia hii ya BVR ni mpya. Lakini mpaka sasa, haijafanyia majaribio nchini. Mitambo hii inahitaji wataalam wa kutosha – kutoka ndani na pengine nje ya nchi.
Haifahamiki kama NEC imetenga fedha za kutosha kwa kazi hiyo. Kinachojulikana, ni malalamiko kuwa serikali imeidhinisha kiasi kiduchu katika mradi huu. Bunge la bajeti limeidhinisha kiasi cha Sh. 7 bilioni, wakati mradi unagharimu kiasi cha Sh. 293 bilioni.
Aidha, kila uchaguzi nchini, NEC hutumia watendaji wa kata, vijiji na halmashauri za wilaya na walimu wa shule za msingi katika kazi ya kuandikisha, kusimamia na kuendesha. Idadi kubwa ya wanaotumwa na NEC katika chaguzi hizo, hawafahamu hata kutumia kompyuta.
Tatu,serikali inakiri kuwapo kwa tatizo la umeme nchini. Lakini inasema, itatumia umeme unaozalishwa kwa njia ya jua. Umeme huu utafungwa kwenye magari maalum.
Hata hivyo, NEC inajua kwamba taifa hili halina miundombinu mizuri ya barabara. Maeneo mengine, hata baiskeli hazifiki. Hivyo basi, kukosekana kwa barabara bora, kutasababisha magari hayo “maalum” kushindwa kufika katika baadhi ya maeneo.
Nne, NEC wanasema, itatumia mtambo wa BVR kuandikisha wapigakura na siyo kupigia kura. Ni utaratibu uleule wa miaka nenda rudi. Lakini wanasema, hawatatumia vidole kumtambua mpigakura.
Sasa swali la kujiuliza: Ikiwa kazi ya BVR ni kuandikisha wapigakura, mfumo huu una faida gani katika kuzuia udanganyifu wakati wa kupiga kura? Mfumo huu utakuwa na faida gani katika kuzuia wapigakura hewa au kuhesabu kura? Utatoa tiba ipi kwa wanaoandikishwa mara mbili?
Wanaoandaa mfumo mpya wa BVR na ambao utameza mamilioni ya shilingi za walipa kodi, hawaoni kuwa tatizo la utambuzi wa mpigakura litabaki pale pale?
Tungeelewa kama mfumo wa BVR ungetumika katika kuandikisha, kuhifadhi na kupiga kura. Ungetumika katika kuzuia watu kujiandikisha mara mbili; na au kuzuia vituo hewa vya kupigia kura.
Lakini kwa hili la sasa, ambako hata yule asiyekuwa na kitambulisho bado aweza kupiga kura, huu ni mradi usiokuwa na tija. Hauhitajiki.
Mashine za mradi huu zimenunuliwa kwa fedha nyingi. Taarifa zinasema, gharama za mashine hizi zimepandishwa zaidi ya mara 10 na genge la wajanja wachache serikalini.

Polepole: Serikali mbili hazitekelezeki




Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Katiba, Humphrey Polepole
Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Katiba, Humphrey Polepole akitoa ufafanuzi juu ya muundo wa Serikali katika Rasimu ya Katiba Mpya


Polepole: Serikali mbili hazitekelezeki

MJUMBE wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humprey Polepole, ameapa kuwa muundo wa Muungano wa serikali mbili hautekelezeki.
Amesema, “Mpango wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuingiza ajenda ya serikali mbili ndani ya rasimu ya katiba, utaweza kuingiza nchi katika matatizo. Hii ni kwa sababu, serikali mbili ndani ya Muungano hazitekelezeki.”
Amesema kupenyeza muundo wa serikali mbili kwenye Bunge la Katiba, ni kiyume cha utaratibu na kuonya kuwa kwa vyovyote itakavyokuwa, “muundo wa serikali mbili ni mgumu na hauwezi kutekelezeka.”
Amesema, “Huwezi kwenda kuwaambia Wanzanzibar wafute vipengele kwenye katiba yao inayotambua Zanzibar ni nchi kamili na Rais wao sio mkuu wa nchi. Halafu wakakuelewa.”
Akizungumza kwa hisia kali kwenye kongamano lililoandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Mtandao wa Wanawake na Katiba Mpya.
Alisema, katiba ya Jamhuri ya Muungano ina muundo wa serikali mbili. Kwa namna matatizo yalivyo, hakuna njia ya kutatua matatizo yaliyosababishwa na muundo huo.
“Zanzibar walitaka Muungano wa mkataba….maana yake ni kuvunja muungano. Lakini baada ya kujadiliana nao, wamesogea kwenye tatu na tunawasihi wengine wasogee hapa kwenye tatu tujadiliane…kitendo cha kubaki huko ni kutaka kuvunja Muungano,”amesisitiza.
Amesema, “Nchi mbili zinapoungana na kuwa na nchi moja; nchi mpya inayozaliwa huwa inapewa mamlaka na madaraka fulani. Nchi mbili zilizoungana zinabaki maeneo ya nchi iliyozaliwa, ambayo huwa yanawekewa utawala wa ndani na sio kuwa na dola huru.
Mkataba huo ulitamka kwamba “ Zanzibar ibaki ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano, lakini itapewa vyombo vya kuratibu masuala ya watanzania waishio Zanzibar kwa ndani. Harafu Jamhuri ya Muungano itashughulika na mambo ya muungano na mambo ya Tanzania bara.”
“Zanzibar na Tanganyika ni maeneo ya Jamhuri . katiba ya Zanzibar ibara ya 1 inasema “ Zanzibar ni nchi” hivi unaweza kuwa na nchi ndani ya nchi nyingine,” amesisitiza